MD Digital

Monday, October 20, 2014

SIMBANET YAFANYA SIKU YA FAMILIA

 Kampuni ya SimbaNET (T) Linited ya jijini Dar es Salaam Jumamosi hii iliandaa bonanza la michezo lililowakutanisha pamoja wafanyakazi wa kampuni hiyo na familia zao. Siku hiyo ilikuwa ni ya kula kunywa na kuchezo michezo ya aina mbalimbali ikiwepo soka, kuvutana kamba, kuogelea, muziki na michezo mbalimbali ya watoto. Kampuni ya Seree ndio walikuwa waandaaji wa tafrija hiyo iliyofanyika kwa mafanikio makubwa katika ufukwe wa Hoteli ya Bahai Beach.
 wafanyakazi na familia zao wakichukua kifuangua kinywa mara baada ya kuwasili bahari Beach Hotel
 
 Hii ni trela tu...
Wafanyakazi wakipata kifungua kinywa.
 Watoto wakifurahia na kushiriki michezo mbalimbali ya kuogelea.
Mgeni rasmi katika siku hiyo ambaye pia ni Mkurugenzi Mkuu wa SimbaNET (T) Limited, Rakesh Kukreja akisalimia wachezaji wa timu zote akifuatana na kamisaa wa michezo hiyo Patrick Nyembela.
 Mchezo wa kuvuta kamba ulifanyika kwa makundi mbalimbali kutokana na fulana walizovaa. na Team ya weupe ndio waliibuka washindi.
 Mchezo wa soka ukiendelea ambapo Afrika Rising 'Fulana za Brown' ndio waliibuka washindi.
 Wafanyakazi kutoka Nairobi wananchi Group nao walialikwa na hapa wakifuatilia michezo hiyo na kubadilishana mawazo.
 Watoto wa wafanyakazi wa SimbaNET wakiogelea.
 Mashindano ya kuogelea nayo yalifanyika na timu ya Afrika Rising ilibuka washindi tena.
 Msosi wa mchana nao uliliwa na ulikuwa wanguvu.
 wafanyakazi wakibadiliashana mawazo.
 Wafanyakazi wakila chakula cha mchana...
 Burudani kutoka Seree Company ilitolewa na kijana chipukizi katika tasnia ya muziki.
 Hapo sasa magoma yakichezwa
 Furaha ya medali kwa African Rising...
 Wow! Keki la Birthday ilikatwa na maana Jovin na Daniela waliadhimisha siku yao ya kuzaliwa hiyo Oktoba 18.
 Burudani ya viongozi wa SimbaNET na wale wa Wananchi Group kutoka Kenya.
 Mkurugenzi wa Seree Company, Sabrina Maro (kulia) akikabidhi tuzo ya shukrani kwa kampyni ya SimbaNET kuipa heshima ya kuwaandalia bonanza hilo lililowakutanisha wafanyakazi na familia zao.
 Wafanyakazi waliopata watoto ndani ya mwaka mmoja tangu kufanyika kwa siku ya familia kama hiyo 2013 walipewa zawadi za aina mbalimbali kwa watoto wao.
Mwisho wafanyakazi na familia zao walipata nyama choma.

No comments: