MD Digital

Thursday, October 23, 2014

PSPF YATOA ELIMU KWA WAJUMBE WA IDARA YA UTUMISHI WA WALIMU NCHINI

Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Adam Mayingu, akisalimiana na baadhi ya wachezaji wa timu ya Polisi Morogoro, Jumatano Oktoba 22, 2014, wakati wa chakula cha jioni kilichoandaliwa na Mfuko huo kwa wachezaji hao na wajumbe wa idara ya utumishi wa walimu, wanaohudhuria semina ya siku moja iliyuoandaliwa na Mfuko huo Mkoani Morogoro, Alhamisi Oktoba 23, 2014
Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Neema Muro, akiwasalimia wajumbe wa semina wakati wa chakula cha usiku kilichoandaliwa na PSPF
Mjumbe wa semina ya siku moja iliyoandaliwa na Mfuko wa Pensehni wa PSPF, kwa wajumbe wa idara ya utumishi wa walimu kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara, akisoma kipeperushi chenye maelezo ya kina ya huduma zitolewazo na mfuko huo, wakati wa semina
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Adam Mayingu, akitoa hotuba ya ufunguzi wa semina ya siku moja kwa wajumbe wa idara ya utumishi wa walimu kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara iliyofanyika mkoani Morogoro leo Alhamisi Oktoba 23, 2014
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Adam Mayingu, akitoa hotuba ya ufunguzi wa semina ya siku moja kwa wajumbe wa idara ya utumishi wa walimu kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara iliyofanyika mkoani Morogoro leo Alhamisi Oktoba 23, 2014
Mtaalamu wa tathmini  wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, James Tenga, akitoa mada kwenye semina hiyo akielezea jinsi tathmini ya mafao inavyofanyika
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Adam Mayingu, (Katikati), akiwasili kwenye ukumbi wa semina ya siku moja iliyoandaliwa na Mfuko huo, kwa wajumbe wa idara ya utumishi wa walimu kutoka mikoa yote ya Tanzania bara, iliyofanyika mkoani Morogoro jana. Semina hiyo ni muendelezo wa Mfuko, kutoa elimu kwa wanachama wake kutoka makundi mbalimbali
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Adam Mayingu, (Kulia), akisalimiana na Hafsa Mrisho, Mkurugenzi wa Utawala na  Rasilimali watu Tume ya Utumishi wa Umma, wakati wa chakula cha jioni kilichoandaliwa na Mfuko huo kwa baadhi ya askari polisi na wajumbe wa idara ya utumishi wa walimu kutoka mikoa ya Tanzania bara wanaohudhuria semina iliyoandaliwa na Mfuko huo mkoani Morogoro jana. Katikati ni Kamanda wa polisi Mkoa wa Morogoro, Leonard Paul
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Adam Mayingu, akizungumza na wajumbe wa idara ya utumishi wa walimu, wakati wa chakula cha usiku kilichoandaliwa na Mfuko huo mjini Morogoro Oktoba 22, 2014. Wajumbe hao wanatarajiwa kubhudhuria semina ya siku moja iliyoandaliwa na Mfuko huo ili kuwaelimisha walimu faida wanazoweza kupata endapo watajiunga na Mfuko huo.
 

Wajumbe wakijaza fomu za kujiunga na mpango wa fao la hiari la Mfuko wa Pensheni wa PSPF, wakati wa semina ya siku moja iliyowakutanisha wajumbe wa idara ya utumishi wa walimu nkutoka mikoa yote nchini na kufanyika mkoani Morogoro Alhamisi Oktoba 23, 2014
Wajumbe wakijaza fomu za kujiunga na mpango wa hiari Mfuko wa Pensheni wa PSPF, wakati wa semina ya siku moja iliyowakutanisha wajumbe wa idara ya utumishi wa walimu kutoka mikoa yote nchini na kufanyika mkoani Morogoro Alhamisi Oktoba 23, 2014
Msanii Mrisho Mpoto, ambaye pia ni balozi wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, akiimba na wasanii wenzake, kwenye hafla ya chakula cha usiku kilichoandaliwa na Mfuko huo kwa wajumbe wa idara ya utumishi wa walimu nchini, wanaohudhuria semina ya siku moja kuhusu huduma mbalimbali zitolewazo na Mfuko huo mkoani Morogoro, Oktoba 23, 2014
Meneja Masoko na Mawasiliano wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Constatina Martin, akiimba sambamba na Msanii Mrisho Mpoto almaarufu kama Mjomba, wakati wa chakula cha usiku kilichoandaliwa na Mfuko huo Jumatano Oktoba 22, 2014, kwa wajumbe wa idara ya utumishi wa walimu, wanaohudhuria semina ya siku moja iliyoandaliwa na PSPF mkoani Morogoro
Meneja wa mpango wa uchangiaji wa hiari wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Mwanjaa Seme, akiswasalimia wajumbe wanaohudhuria semina ya siku moja iliyoandaliwa na Mfuko huo, kwa wajumbe wa idara ya utumishi wa walimu semina iliyofanyika mkoani Morogoro Oktoba 23, 2014

No comments: