MD Digital

Monday, June 15, 2015

JAMII ISHIRIKIANE KATIKA MALEZI YA WATOTO



JUNI 16 ya kila mwaka bara la Afrika huadhimisha siku ya mtoto wa  Afrika ikiwa ni tukio la kuwaenzi na kuwakumbuka watoto wa Soweto nchini Afrika Kusini waliofariki wakati wa maandamano ya kutaka haki na usawa katika elimu kutoka utawala wa Makaburi mwaka 1976.

Ni Umoja wa Nchi huru za Afrika (OAU) hivi sasa Umoja wa Afrika (AU) mwaka 1991 ndio waliamua kuifanya siku hiyo kuwa ya kuwakumbuka na kuwaenzi wa watoto wa Afrika kwa maadhimisho ya kitaifa na kimataifa ambayo yanafanyika kwa kuzungumzia haki za mtoto.

Huu ni mwaka wa 24 tangu AU iidhinishe siklu hiyo ya mtoto wa Afrika kuadhimishwa, lakini pia ni mwaka wa 39 tangu watoto wa Soweto wapoteze maisha yao wakati wakidai haki yao.

Mwaka jana maadhimisho hayo yalikuwa na kaulimbiu ya “Haki ya Ushiriki: Waache watoto waonekane na wasikike” na mwaka huu pia kuna kauli mbiu yake ambayo inaogoza maadhimisho hayo hii leo.

Pia maadhimisho ya mwaka huu yanafanyika wakati Wakuu wa Nchi za Afrika chini ya Umoja wao AU wanakutana nchini Afrika kusini ambapo miaka 39 iliyopita palitokea vuru na watoto kuuwawa.

Siku ya Mtoto wa Afrika mwaka huu inafanyika   sambamba na maadhimisho ya Miaka 25 ya Kupitishwa kwa Mkataba wa Haki za Mtoto wa Afrika na kaulimbiu ya mwaka huu ni: “Kuongeza Kasi na Jitihada Zetu za Pamoja Kutokomeza Ndoa za Utotoni Afrika.”

Kama mzazi ambaye nami ni nawatoto wa kike na hata wakiume pia ninaunga mkono kauli mbiu ya mwaka huu.

Mimba za utotoni katika nchi nyingi za Afrika bni tatizo kubwa ambalo hakika linahitaji sauti ya pamoja ya kulikemea ili kuliondoa kama si kulimaliza kabisa.

Vita vya mara kwa mara katika nchi nyingi za Afrika ni moja ya vitu ambavyo husabisha watoto wengi wa kike kupata mimba za utotoni kutokana nakubakwa na hata wengine kunajisiwa.

Lakini hapa Tanzania sisi tuna amani ya kutosha na utulivu ambao kama tutautumia ipasavyo hili tunaliweza kuliondoa achilia mbali umasikini unaozikabili kaya zetu na kupelekea watoto hasa washule kulubuniwa na malaghai wachache na kuishia katika mimba.

Lakini wapo wazazi waliokosa hekima na busara ambao huwaoza binti zao wakiwa na umri mdogo na wengine hata bila kuwashirikisha watoto hao.

Jana Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake (Tamwa) kupitia Mkurugenzi Mtendaji wa wake, Valerie Msoka, walitoa tamko na kusema kuwa ni ukiukwaji wa haki za mtoto wa kike kutokana na kuwa ndoa nyingi zinapangwa na kujikita zaidi katika makubaliano kati ya anayetaka kuoa na wazazi wa mtoto wa kike na kushindwa kuhakikisha mhusika mkuu anaridhika.

Msoka alisema kuwa ndoa za umri mdogo zimeonesha kuongezeka kwa kipindi cha miaka 10 iliyopita ambapo takwimu zinaonesha kuwa barani Afrika na Asia vitendo hivyo vinaongoza.

Utafiti wa Watu na Afya nchini Tanzania (TDHS) wa mwaka 2010, ulibawastani wa watoto wanne katika kila watoto 10 wa kike wanaolewa kabla ya kufikia umri wa miaka 18.

Kwa mujibu wa utafiti huo, inakadiriwa kuwa asilimia 37 ya wanawake wa umri kati ya miaka 20 na 24 kwa mwaka 2000/2011 waliolewa au kuwa na mahusiano ya ndoa walipofikia umri wa miaka 18.

Mmomonyoko wa maadili katika jamii ndio chanzo kikubwa pia ya kukosekana kwa maadili ambayo yanapelekea watoto wetu hawa kuingia katuika vitendo hivyo kabla ya wakati.

Ndoa zinapokuwa na migogoro ambapo baba na mama wanakosa kuelewana kama kuna mtoto wa kike na kiume basi watoto wa kike huishia kuozwa katika umri mdogo kwa tama ya mzazi mmoja.

Hivyo basi ni vyema wazai tukadumisha amani katika ndoa zetu na kuwapa malezi mema watoto wetu ili wakue kwa misingi iliyobora.

Umefika wakati sasa wa jukumu la malezi ya watoto wetu kuto liacha kwa wazazi pekee bali liwe la jamii nzima kama ambavyo sisi tulilelewa hapo zamani na tukakua kwa maadili. (Porojo hii pia imechapishwa katika gazeti la Habarileo Juni 16,2015 kama WAZO).

No comments: